Kuna faida nyingi za kupata kula chakula bora, chache kati yake ni hizi:
Chanzo cha virutubisho
Kupata chakula bora kunaupa mwili virutubisho muhimu kwa afya na kujilinda na magonjwa. Mwili una uwezo wa kutengeneza virutubisho vingi, lakini kuna baadhi lazima vipatikane kutokana na chakula.
Kupungua uzito
Kuwa na uwiano mzuri kati ya mwili na uzito (au Body-Mass-Index BMI) ni kitu muhimu katika kuhakikisha afya yako iko sawa. Ukila chakula bora unahakikisha unapata virutubisho muhimu ili kuupa mwili wako uwezo wa kujiweka sawa na kutoongezeka uzito bila sababu.
Kuboresha kinga ya mwili
Mwili hufanya kila kitu kutokana na virutubisho vinavyopatikana. Kula chakula bora huupa mwili kiwango kizuri cha virutubisho vinavyohitajika ili kuimarisha mfumo wa kinga dhidi ya magonjwa.
Kuusaidia mwili kujijenga vizuri
Chukulia chakula kama dawa za kuutibu mwili. Chakula kizuri huupa mwili virutubisho vizuri ziadi na kuufanya uwe bora. Seli za mwili hujengeka kutokana na virutubisho vinavyopatikana kwenye chakula. Kukoseakana kwa aina fulani ya virutubisho hufanya seli za mwili kuwa dhoofu hivyo kutokuwa na siha njema.
No comments:
Post a Comment